Mbunge wa Pangani (CCM), Jumaa Aweso, amefanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani na kukutana na upungufu kadhaa.Ziara ya mbunge huyo hospitalini hapo, ilikuwa na lengo la kukagua uwajibikaji wa watumishi pamoja na changamoto wanazokutana nazo.Aweso baada kutembelea kila kitengo hospitalini hapo, alieleza kutoridhishwa na huduma zinazotolewa katika na kwamba zina upungufu mwingi ikilinganishwa na mategemeo ya wananchi kwa kuwa ndiyo hospitali kubwa wilayani hapo.Alitaja baadhi ya upungufu aliokutana nao ni pamoja na kutofanya kazi kwa mashine ya x-ray na baadhi ya mashine za maabara, jengo la upasuaji kuvuja na uhaba wa vifaa tiba.Kutokana na hali hiyo, alisema atawasilisha kunakuhusika ili serikali ichukue hatua za haraka kunusuru maisha ya wananchi wa wilaya hiyo.Aweso alieleza kushangazwa na uchakavu wa jengo la upasuaji hadi kufikia hatua ya kuvuja pamoja na kukosekana kwa vifaa hivyo muhimu na kudai kuwa hali hiyo licha ya kutishia maisha ya jamii, pia ni mzigo kutokana na kulazimika kwenda mbali kufuatahuduma hizo.Mbunge huyo aliahidi kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya kupitia mfuko wa jimbo kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi mara moja.Kwa upande wake, aliahidi kuwashirikisha wadau mbalimbali wa Pangani ili kuhakikisha kitengo cha upasuaji kinaimarishwa haraka ili kupunguza kama si kumaliza kabisa tatizo la kukosekana kwa hudumahiyo.Aweso alitumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wa Pangani kujiunga mfuko wa bima ya afya ili kupata matbabu kwa urahisi kwa kuwa kufanya hivyo kutapunguza gharama kwa wananchi wengi ambao wengi wao hawana uwezo wa kiuchumi.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni