Serikali imesema kukosekana kwa fedha za kutosha kumechangia baadhi ya miradi ya maendeleo kusimama ikiwano ya barabara.Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani, wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali, aliyetaka kujua ni lini serikali itapeleka fedha kwa mkandarasi ili aweze kumaliza ujenzi wa daraja la Kilombero.Ngonyani alisema fedha za ujenzi wa daraja hilo zinatolewa na serikali kwa asilimia 100 lakini haiwezi kukamilisha miradi yote kwa wakati mmoja kutokana na uwezo wa mdogo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani.Alisema ujenzi wa daraja hilo unatarajia kukamilika Desemba mwakahuu.Akijibu swali la msingi lililohoji ni lini seriklai itaanza kumaliza ujenzi wa barabara ya Kidatu, Ifakara na Mlimba kwa kiwango cha lami.Alisema barabara ya Kidatu hadi Ifakara mradi huo umeanza kutekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha na katika awamu ya kwanza naya pili jumla ya kilomita 16.17 zilijengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni