Watanzania acheni kushabikia mambo yasiyo na faida. - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Ijumaa, 7 Novemba 2014

Watanzania acheni kushabikia mambo yasiyo na faida.

 

Nianze kwa kuwapa salamu Watanzania wenzangu mliojaa uzalendo, mlio tayari kuhoji mambo ya msingi kwa mustakabali wa nchi yetu.
Nawapongeza kwa sababu mnajitambua na angalau mnaweza kuwatia kashikashi viongozi wa Serikali pale ambapo wanasahau majukumu yao.
Nia yangu si kuponda tabia za baadhi ya Watanzania wenzagu ‘waliolala’, lengo langu ni kuwapa ushauri tu kwamba hata kama wanashabikia mambo yasiyo na faida katika maisha yao, wakumbuke kuwa kuna mambo ya muhimu yanahitaji kupigiwa kelele kama si kupingwa.
Wananchi ndio wenye nchi, hivyo wanapaswa kuhakikisha kuwa nchi yao ipo katika njia sahihi. Hata nchi zilizoendelea zilifikia hatua hiyo baada ya wananchi wake kujitambua.
Hapa kwetu Tanzania baadhi ya wananchi wamekuwa mahodari kuhoji na hata kufuatilia, mambo ambayo hayawezi kuwasaidia hata kupata mlo wa usiku tu.
Kila mtu analikumbuka lile sakata la Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu. Mwanadada huyu aliyetwaa taji la urembo, anakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kudanganya umri wake, kitu ambacho ni kinyume na kanuni za mashindano hayo ya urembo.
Sakata hilo lilikuwa mjadala katika mitandao ya kijamii, vijiweni, katika daladala na hata kwenye baadhi ya maofisi.

Ni kweli kabisa mrembo huyo wa Tanzania anakwenda kuiwakilisha nchi, lakini tujiulize nguvu iliyotumika kumpinga Sitti ina faida gani kwa wananchi maskini.
Umejaribu kufikiri Miss Tanzania inasaidiaje kuboresha maisha yako na wananchi wengine walioko vijijini. Miss Tanzania inaweza kuleta huduma bora za afya?
Vipi kuhusu elimu, unadhani Miss Tanzania inaweza kuisaidia nchi kujenga mabweni, maabara, kununua madawati. Jibu ni hapana.
Mambo niliyoyataja hapo juu ni baadhi tu yanayotakiwa kupigiwa kelele na idadi kubwa ya Watanzania ili kuifanya nchi yetu iweze kupiga hatua kama nchi nyingine ambazo miaka 1960 zilikuwa hazina tofauti ya kiuchumi na Tanzania.
Sikatai watu kumpinga, kinachonishangaza ni tabia ya walio wengi ya ‘kushupalia’ jambo hili au mengine yanayofanana na hilo huku wakiacha kujadili mengine ya msingi.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa