Rais wa Nicaragua amchagua mkewe kuwa mgombea mwenza - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Jumatano, 3 Agosti 2016

Rais wa Nicaragua amchagua mkewe kuwa mgombea mwenza

Rais wa Nicaragua Daniel Ortega amemtaja mkewe kama mgombea mwenza na makamu wa rais wakati huu ambapo anawania kuchaguliwa kwa muhula mwengine.

Mkewe Rosario Murillo tayari ana wadhfa maarufu wa msemaji waserikali na anaonekana kuwa anagawana mamlaka na mumewe.

Amekuwa akionekana katika runinga ya Nicaragua kila sikuWakosoaji wanawashtumu wanandoa hao wawili kwa kuiendeshaNicaragua ambayo inakabiliwa na uchaguzi mkuu mwezi Novemba kama chombo chao cha kibinafsi.

Rais Ortega akiwa hazungumzi sana katika vyombo vya habari,mkewe huonekana mara kwa mara katika runinga akijadili sera nakujikuza .

Akiwa mama wa watoto 7 wa rais huyo anajua kuongea Kiingereza na Kifaransa huku akijulikana pia kuwa mshairi.

Pia anasifa za kuvaa mavazi yenye rangi nyingi na vito vya miakaya sitini.

Wanahabari wanasema kuwa raia wengi wa taifa hilo wanamuona bi Murillo kama mwenye uwezo mkubwa katika taifa lake kutokana na hadhi yake katika uma.

Mume na mkewe waliwasilisha makaratasi yao ya kugombea viti hivyo rasmi katika mji mkuu wa Managua wakiandamana na mshauri wakili wa chama chao cha Sandinista.



ni kazi yangu kukujuza

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa