Katika kumuunga mkono Rais Dk. John Magufuli kutekeleza mpango wa elimu bure, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na viongozi wa vyama vya usafirishaji abiria jijini Dar es Salaam, wameamua walimu wa shule za msingi na sekondari kuanzia Machi 7, mwaka huu, kutolipa nauli katika daladala.Mpango huo utaanza kutumika baada ya kukamilika utengenezaji wa vitambulisho maalumu kwa waalimu hao wanaokadiriwa kuwa 10,000.“Ninawatangazia wananchi kuwa kuanzia Machi 7, mwaka huu, walimu wa sekondari na msingi watasafiri bure katika vyombo vya usafiri katika jiji letu la Dar es Salaam,” alisema Makonda.Mwenyekiti wa Chama cha Wasafirishaji Dar es Salaam (Darcoboa), Sabri Mabruki, alisema makubaliano hayo ni kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Magufuli katika kutekeleza mpango wa elimu bure na kupunguza makali ya maisha kwa walimu hao.Alisema walimu wataanza kusafiri bure kuanzia saa 11:30 alfajiri hadi saa mbili asubuhi, na saa 9 alasiri hadi saa 11 jioni. Nje ya muda huo, alisema watalazimika kujilipia.“Tujifunze tunapomuona kiongozi kijana anapopenda maendelea inatubidi tumuunge mkono. Makonda tangu aingie Kinondoni ameonyesha nia yadhati ya kuleta maendeleo,” alisema Mabruki.Alisema walimu wote watasafirishwa kwa utaratibu wa vitambulisho na kuwapo na utaratibu wa kila garikuingia walimu wachache.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni