Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amewasimamisha kazi na kuwastaafisha maofisa watatu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kwa tuhuma za kuhujumu mtambo wa mawasiliano na kuisababishiaserikali hasara ya Sh. bilioni nne.Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu, Profesa Mbarawa aliwataja maofisa hao kuwa ni Mkurugenzi wa Sheria wa TCRA, Elizabeth Nzagi, Mwanasheria Modester Ndunguru na aliyekuwa msimamizi wa mtambo huo, Mhandisi Richard Sunday.Alisema kuna kifaa cha kubaini gharama za mawasiliano ya kila simu nchini ili kujua kampuni zinapata kiasi gani kilipaswa kufungwa kwa muda mrefu, lakini hakikufugwa kwa sababu zisizojulikana.“Mkataba ulisema kifugwe ili tujue gharama za mawasiliano lakini hakikufugwa na badala yake kujua gharama imetegemea kampuni za simu pekee, huku simu za nje serikali ikijua gharama husika,” alisema.Alisema maofisa hao watakuwa nje ya vituo vyao vya kazi wakati uchunguzi ukiendelea kwa hatua zaidi.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni