Dar: RC Makonda kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wanaume zao - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Ijumaa, 23 Machi 2018

Dar: RC Makonda kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wanaume zao



Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewatangazia wawanake wote waliotelekezwa na waume zao na hawapatiwi fedha za matunzo ya mtoto kufika ofisini kwake siku ya Jumatatu ya April 09 kwaajili ya kupatiwa msaada wa kisheria.
    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya RC, inasema Jopo la wataalamu wa Sheria, Maafisa Ustawi wa jamii na Askari Polisi kutoka Dawati la Jinsia wamejipanga ipasavyo kukuhudumia na kuhakikisha mzazi mwenzio anatoa fedha za matunzo ya Mtoto.

“Ewe mwanamke huu sio wakati wa kulia wala kuteseka, serikali yako itasimama na wewe kuhakikisha unapata haki yako uliyoikosa kwa muda mrefu,” Taarifa hiyo inaeleza.

Alisema Huduma hii inatolewa bure chini ya uongozi thabiti wa serikali ya awamu ya tano.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa