Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (pichani), ameiagiza Kamati ya Uchumi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu ikutane na wafanyabiashara wote ili wajadiliane na kupanga kiwango cha ushuru kinachopaswa kutozwa kwenye mazao ya wilaya hiyo.Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana, wakati akizungumza na mamia ya wananchi waliofika kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Dutwa, wilayani hapa.Alitoa agizo hilo baada ya kuona bango lililoshikwa na wananchi wakilalamikia kutozwa ushuru wa Sh. 3,000 kwa gunia moja la mazao badala ya Sh. 1,000 ya zamani.Alisema masuala ya ushuru ni maamuzi baina yao na Halmashauri, lakini hiyo tozo imeongezwa sana, hivyo kuagiza kamati hiyo na wafanyabiashara wakutane kujadili suala hilo na wakubaliane kiwangocha ushuru.Alisema: “Wabunge pia waalikwe kwenye kikao hichona Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Baraza laMadiwani nalo pia lishiriki. Kama mnataka kupandisha ushuru ni lazima mkubaliane viwango ili Watanzania wafanye biashara wakiwa na mapenzi na nchi yao.”Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema suala la kulipa ushuru ni la muhimu katika kuchangia makusanyo ya kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi. “Ushuru ni lazima ulipwe, lakini pia ni lazima muwe mmekubaliana ni kiwango gani mnatoza,” alisema Majaliwa.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewazuia maofisa kutoza ushuru na kudai fedha kabla mwananchi hajauza mifugo wanapoipeleka mnadaniakisema kuwa wanakuwa wamekwenda kutafuta fedha.Alifanya uamuzi huo wakati akijibu hoja iliyotolewa na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Gimbi Masabo, ambaye alimweleza Waziri Mkuu kwamba kuna tabia ya kutoza Sh. 6,000 kwa kichwa kwa kila ng’ombe anayeswagwa kuingia eneo la mnada bila kujali kama mtu huyo ameuza ng’ombe au la.Alimwagiza Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, RobertLweyo, aimarishe usimamizi wa minada na kujua idadi ya mifugo ambayo inaingizwa, inayouzwa na ile inayobaki ambayo imeshindikana kuuzwa.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni