Waziri Mkuu aagiza kikao kujadili ushuru wa mazao. - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Jumamosi, 5 Machi 2016

Waziri Mkuu aagiza kikao kujadili ushuru wa mazao.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (pichani), ameiagiza Kamati ya Uchumi ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu ikutane na wafanyabiashara wote ili wajadiliane na kupanga kiwango cha ushuru kinachopaswa kutozwa kwenye mazao ya wilaya hiyo.Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana, wakati akizungumza na mamia ya wananchi waliofika kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Dutwa, wilayani hapa.Alitoa agizo hilo baada ya kuona bango lililoshikwa na wananchi wakilalamikia kutozwa ushuru wa Sh. 3,000 kwa gunia moja la mazao badala ya Sh. 1,000 ya zamani.Alisema masuala ya ushuru ni maamuzi baina yao na Halmashauri, lakini hiyo tozo imeongezwa sana, hivyo kuagiza kamati hiyo na wafanyabiashara wakutane kujadili suala hilo na wakubaliane kiwangocha ushuru.Alisema: “Wabunge pia waalikwe kwenye kikao hichona Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Baraza laMadiwani nalo pia lishiriki. Kama mnataka kupandisha ushuru ni lazima mkubaliane viwango ili Watanzania wafanye biashara wakiwa na mapenzi na nchi yao.”Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema suala la kulipa ushuru ni la muhimu katika kuchangia makusanyo ya kodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi. “Ushuru ni lazima ulipwe, lakini pia ni lazima muwe mmekubaliana ni kiwango gani mnatoza,” alisema Majaliwa.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewazuia maofisa kutoza ushuru na kudai fedha kabla mwananchi hajauza mifugo wanapoipeleka mnadaniakisema kuwa wanakuwa wamekwenda kutafuta fedha.Alifanya uamuzi huo wakati akijibu hoja iliyotolewa na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Gimbi Masabo, ambaye alimweleza Waziri Mkuu kwamba kuna tabia ya kutoza Sh. 6,000 kwa kichwa kwa kila ng’ombe anayeswagwa kuingia eneo la mnada bila kujali kama mtu huyo ameuza ng’ombe au la.Alimwagiza Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, RobertLweyo, aimarishe usimamizi wa minada na kujua idadi ya mifugo ambayo inaingizwa, inayouzwa na ile inayobaki ambayo imeshindikana kuuzwa.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa