Mdee ahojiwa kwa saa sita, alala rumande. - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Jumatano, 2 Machi 2016

Mdee ahojiwa kwa saa sita, alala rumande.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee, amehojiwa kwa saa sita na baadaye kulazwa rumande na Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam.Mbunge huyo ambaye jana mchana alikamatwa na polisi nyumbani kwake baada ya kuizunguka kwa saa kadhaa, anashikiliwa kutokana na vurugu zilizotokea Februari 27, mwaka huu kwenye ukumbi wa Karemjee baada ya uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam kuahirishwa kwa kile kilichoelezwa ni kutokana na zuio la mahakama.Mbali na Mdee, watu wengine watatu wakiwamo Diwani  wa Kata ya Saranga, Efraim Kinyafu na Diwani wa Kata ya Mbezi, Hamfrey Sambo wote wa Chadema na kada wa chama hicho kata ya Mabibo, Shafii Juma, wanashikiliwa na polisi kuhusiana na vurugu hizo.Baada ya polisi kuzunguka nyumba yake, Mdee alikataa kuondoka kwa magari ya polisi na badala yake akatumia gari lake kwenda  Ofisa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam.Baada ya kufika kwenye kituoni hapo saa  7:20 mchana, mbunge huyo alihojiwa mpaka saa 12:54 polisi walipoamua kumlaza rumande.Awali, askari polisi sita walifika nyumbani kwa Mdee,maeneo ya Makongo, majira ya saa 2:00 asubuhi na kuomba kumchukua ili kuondoka nae.Shuhuda wa tukio hilo ambaye pia ni mmoja wa familia ya Mdee, alisema askari hao ambao waliokuwa wamevalia nguo za kiraia walimtuma kijana waliyemkuta nje ya nyumba kuwa wanamuhitaji mbunge huyo kwa mahojiani."Kijana yule kumbe hakumfikishia taarifa Mdee na askari walikaa nje kwa takribani saa mbili hadi majira ya saa 4:00 asubuhi alipokwenda kijana mwingine kumfuata na kutoka nje," alisema shuhuda huyo.Alisema baada ya Mdee kutoka aliwahoji askari hao sababu ya kujazana nyumbani kwake nao walieleza kuwa walitumwa na Jeshi la Polisi kumkamata kwa mahojiano."Walikuwa hawana barua ya kumkamata ndipo Halima (Mdee) alipowafukuza na kuwaambia kama hawana barua wakachukue ndio wanaweza kwenda naye au wampigie simu yeye binafsi aende polisi badala ya kumkamata," alisema shuhuda huyo.Alisema baadae majira ya saa 5:45  asubuhi, askari hao wakiwa na barua walimchukua Mdee na kuongozana naye hadi Kituo cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano kuhusuiana na vurugu zilizotokea siku ya uchaguzi wa Meya mwishomi mwa wiki iliyopita.Wakili wa Mdee, Prof. Abdallah Safari,  aliwaambia waandishi wa habari kwamba, polisi wanamuhusisha Mdee na kumpiga aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi huo Theresia Mmbando, ingawa walisema hawana ushahidi wa suala hilo.Alisema anawashangaa polisi hao kumlaza Mdee ndani wakati ni Mbunge anaruhusiwa kujidhamini mwenyewe na kwamba kosa linalomkabili haliwezi kumfanya alale rumande.Baadhi ya watu waliokuwa kituoni hapo walisema,   Mdee pia anadaiwa kuchukua nyaraka za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wakati wa vurugu za uchaguzi.Chanzo kimoja cha habari kiliimbia Nipashe kuwa, wafuasi wengine wa Chadema wanahojiwa kutokanana kuhusishwa na vurugu hizo pamoja na kumshambulia Mmabando.Kwa mujibu wa Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Said kubenea,  madiwani hao waliitwa kituoni hapo kwa ajili ya kuhojiwa kuhusiana na vurugu za uchaguzi wa Meya wa jiji.Alisema  akiwa kituoni hapo kwa shughuli nyingine za kufungua kesi, alipata taarifa kuwa mwingine  anayetafutwa ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga, MwitaWaitara, ambaye hadi jana jioni alikuwa hajafika kituoni hapo.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa