Mwanasiasa mkongwe Zanzibar, Ali Ameir Mohamed, amesema Zanzibar ni nchi huru inayojitegenea ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo haipaswi kuingiliwa wala kuhojiwa katika mambo yake ya ndani, ikiwamo suala la kurudiwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar utakaofanyikaMachi 20, mwaka huu.Akizungumza na Nipashe mjini hapa jana, Ali Ameir alisema Zanzibar ina madaraka yake, katiba yake, Rais wake, Baraza la Wawakikishi na mahakama, hivyo haipaswi kuingiliwa katika mambo yake licha ya kuwa shemu ya Tanzania.Alitoa kauli hiyo baada ya kutolewa kwa tamko la nchi saba za Jumuiya ya Ulaya zikiongozwa Marekani, kuwa hawajaridhishwa na kurudiwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar.Alisema mabalozi wanaowakilisha mataifa yao nchini lazima wafahamu na kutambua kuwa Zanzibar ni nchi huru na ilipata uhuru wake uliootokana na Mapinduzi yaliouangusha ufalme wa kigeni uliokalia visiwa hivyo kwa miaka 160.Alisema kitendo cha mabalozi wa nchi nyingine kuhoji uamuzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kutangaza kurudia uchaguzi ni kuingilia mambo ya ndani ya Zanzibar, kwenda kinyume cha taratibu za kidiplomasia na ukiukaji wa mikataba ya kimataifa.Alisema katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 imeipa mamlaka ZEC kuratibu, kuitisha, kusimamia na kutangaza matokeo ya uchaguzi na kwamba maamuzi yake hayawezi kuhojiwa au kuingiliwa na mtu au mamlaka yoyote iwe ya ndani au nje ya nchi.Alisema uamuzi uliofanywa za ZEC kuitisha uchaguzi wa marudio unapaswa kuheshimiwa kwa sababu yanatokana na utashi wa katiba na sheria nakwamba hiyo ndiyo njia pekee ya kukwamua utata wa mkwamo wa uchaguz mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni