Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeshindwa kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na waliokuwa makada wa CCM, Mgana Msindai na John Guninita (kwa sasa ni makada wa Chadema) dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paulo Makonda, baada ya kukosekana kwa projekta ya kuonyesha picha zilizorekodiwa siku ya tukio.Wakili wa walalamikiwa Benjamin Mwakagamba alidai mbele ya Hakimu Mkazi Hellen Riwa kwamba, kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa jana ushahidi wa Guninita, lakini ushahidi wake utahusisha kielelezo cha CD lakini kwa kuwa hawakuwa na projekta aliomba tarehe nyingine ya kusikilizwa.Aidha aliiomba mahakama kuwapatia muda wa siku 14 kwa ajili ya kufanya maandalizi ya kutafuta projekta ya kuonyesha tukio mahakamani.Hakimu Riwa alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa ushahidi wa Guninita Februari 15, mwakahuu.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni