Mafuta ya taa, mirungi vyanaswa vikiingizwa kwa njia za panya. - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Jumanne, 16 Februari 2016

Mafuta ya taa, mirungi vyanaswa vikiingizwa kwa njia za panya.

Mafuta ya taa lita 1,200 na kilo 98 za dawa za kulevya aina ya mirungi, vimekamatwa vikiwa katika harakati za kuingizwa nchini kwa njia za panya katika mpaka wa Tanzania na Kenya wa Horohoro.Bidhaa hizo ambazo zilikuwa zikiingizwa kwa njia zamagendo, zilikamatwa katika pori lililo karibu na mpaka huo.Kukamatwa kwa mafuta na mirungi hiyo, kunatokanana kazi maalumu iliyofanywa na timu ya maofisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Idara ya Uhamiaji, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) kwalioko katika mpaka wa Horohoro.Ofisa wa TRA, Edwin Iwato, alisema operesheni hiyo ilifanyika kwa lengo la kukabiliana na mitandao ya uhalifu kupitia mpakani, sambamba na kuwakamata na kuwachukulia hatua wafanyabishara wanaotumianjia za panya ili kukwepa kodi.Iwato alisema kwa sasa watendaji kutoka idara mbalimbali zinazofanya kazi kwenye mpaka huo, wamejiwekea utaratibu wa kuhakikisha wanapambana na uhalifu huo, kutokana na kukithiri kwa vitendo vya uvunjaji wa sheria za nchi, ikiwamo uingizaji holela wa wahamiaji haramu, dawa za kulevya na bidhaa za magendo.“Operesheni hii ni maalum katika kupambana na wahalifu hawa na huu ni mwanzo tu lakini itakuwa endelevu. Watakaobainika kuhusika na vitendo hivi, watafikishwa kwenye vyombo vya sheria,” alisema.Kwa upande wake, Mrakibu Mwandamizi wa Idara ya Uhamiaji Kituo cha Horohoro, Mwesiga Lubalila, alisema bidhaa hizo zilikamatwa baada ya wahusikakubaini mtego uliokuwa umewekwa. Alisema wahusika walipobaini kuwa wanafuatiliwa, walipotupa pikipiki na kukimbia.“Kundi la watu waliokuwa na pikipiki zilizobeba maboksi, walipobaini mtego wa kukamatwa walizitupa pikipiki na kisha kukimbia.Tulipopekua tulikuta dawa za kulevya aina ya mirungi zenye uzito wa kilo 98 zilizokuwa zimefungwa katika vifurushi vyenye uzito wa kilo moja moja,” alisema.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa