Kuna uwezekano mwili wa aliyekuwa Mbunge wa VitiMaalum (Chadema), Leticia Nyerere, aliyefia nchini Marekani utawasili nchini mapema kwa ajili ya maziko tofauti na ratiba iliyokuwa imepangwa awali.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa familia ya Mwalimu Nyerere, Rose-Mary Nyerere, alisema Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilson Masilingi, kwa kushirikiana na familia hiyo wanafanya jitiahada kuusafrisha mwili huo kuja nchini kabla ya Jumatatuiliyokuwa imepangwa awali.“Ratiba inaonyesha mwili utawasili nchini Januari 18kulingana na taratibu za safari, ila tunajaribu kuangalia njia ya kufupisha muda huo kwa sababu nimbali tangu mpendwa wetu Leticia alipotutoka,” aliasema.Alisema mwili huo baada ya kuwasili nchini utaagwa nyumbani kwa Mwalimu Nyerere, Msasani, jijini Dar es Salaam na taratibu za kuusafirisha kwenda kijijini Butiama, mkoani Mara kwa ajili ya maziko zitaendelea.Miongoni mwa viongozi wa serikali waliofika jana nakutoa rambirambi kwa familia ya Nyerere ni Spika wa Bunge, Job Ndugai.Leticia alifariki dunia katika Hospitali ya Doctors Community iliyopo Lan ham, Maryland, nchini Marekani na msiba nchini humo upo DMV 9004 Brightlea Court, Lanham, MD 20706.Marehemu ameacha watoto watatu, wawili wa kike na mmoja wa kiume.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni