Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM), kimeitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi mkuu wa marudio na vilivyojiondoa kabla ya kufanyika uchaguzi huo Machi 20, mwaka huu.Msimamo huo ulitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, Ofisi Kuu za CCM Kisiwanduwi, baada ya vyama vinane kutangaza kuwa vimejiondoa.Vuai alisema ZEC inapaswa kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi wa marudio pamoja na vile vilivyojiondoa baada ya muda wa kuthibitisha kushitiki kumalizika Febuari 11, mwaka huu.Alisema kuna baadhi ya wanasiasa wameanza kufanya vitendo vya udanganyifu kuwa hawatashirikiuchaguzi wa marudio wakati uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana, hawakusimamisha wagombea.Vuai alisema viongozi wa vyama vya UPDP na UMD wamekuwa wakiwadaganya wananchi na dunia kuwa hawatoshiriki uchaguzi wa marudio wakati hawakuwa na wagombea katika uchaguzi wa Oktoba25.“Kuna utapeli wa kisiasa unafanyika, utasema vipi umejitoa katika uchaguzi wakati hukusimamisha wagombea katika uchaguzi uliyofutwa na Tume ya Uchaguzi mwaka jana,hii ni hadaa na hila .”alisema Vuai.Hata hivyo alisema kuwa kujiondoa kwa baadhi ya vyama hakuna madhara wala upungufu wowote katika uchaguzi huo kwa kuwa suala la kushiriki au kutoshiriki ni jambo la hiari.Taarifa ya CCM imekuja baada ya vyama vinane vya siasa kutangaza hawatoshiriki uchaguzi wa marudio vikitala taarifa zao kuondolewa katika karatasi za wapiga kura kwa madai uchaguzi wa Oktoba 25 ulikuwa huru na wa haki.Vyama hivyo ni Chauma, CUF, DP, Demokrasia Makini, SAU, Jahazi Asilia, NRA pamoja na UPDP naUMD ambavyo havikuwa na wagombea.Kuhusu hatima ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Vuai alisema itajulikana baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio.Alisema pamoja na CUF kujitoa, bado vyama vingine vina nafasi ya kushirikishwa katika serikali hiyo ikiwa vitapata nafasi ya kukidhi matakwa ya kikatiba na kisheria baada ya kuchaguliwa na wananchi na kupata uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.Hata hivyo, alisema kuwa CCM ipo tayari kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa na chama chochote ambacho kitatimiza mashariti ya Katiba ya kupata zaidi ya asilimia 10 ya matokeo ya uchaguzi. - MKWELI BLOG

Karibu kwenye kitovu cha HABARI.

PATA HABARI ZA MICHEZO KUTOKA KILA KONA YA DUNIA NA MAGAZETI KWA WAKATI UKIWA KARIBU NASI

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Jumanne, 16 Februari 2016

Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM), kimeitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi mkuu wa marudio na vilivyojiondoa kabla ya kufanyika uchaguzi huo Machi 20, mwaka huu.Msimamo huo ulitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, Ofisi Kuu za CCM Kisiwanduwi, baada ya vyama vinane kutangaza kuwa vimejiondoa.Vuai alisema ZEC inapaswa kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi wa marudio pamoja na vile vilivyojiondoa baada ya muda wa kuthibitisha kushitiki kumalizika Febuari 11, mwaka huu.Alisema kuna baadhi ya wanasiasa wameanza kufanya vitendo vya udanganyifu kuwa hawatashirikiuchaguzi wa marudio wakati uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana, hawakusimamisha wagombea.Vuai alisema viongozi wa vyama vya UPDP na UMD wamekuwa wakiwadaganya wananchi na dunia kuwa hawatoshiriki uchaguzi wa marudio wakati hawakuwa na wagombea katika uchaguzi wa Oktoba25.“Kuna utapeli wa kisiasa unafanyika, utasema vipi umejitoa katika uchaguzi wakati hukusimamisha wagombea katika uchaguzi uliyofutwa na Tume ya Uchaguzi mwaka jana,hii ni hadaa na hila .”alisema Vuai.Hata hivyo alisema kuwa kujiondoa kwa baadhi ya vyama hakuna madhara wala upungufu wowote katika uchaguzi huo kwa kuwa suala la kushiriki au kutoshiriki ni jambo la hiari.Taarifa ya CCM imekuja baada ya vyama vinane vya siasa kutangaza hawatoshiriki uchaguzi wa marudio vikitala taarifa zao kuondolewa katika karatasi za wapiga kura kwa madai uchaguzi wa Oktoba 25 ulikuwa huru na wa haki.Vyama hivyo ni Chauma, CUF, DP, Demokrasia Makini, SAU, Jahazi Asilia, NRA pamoja na UPDP naUMD ambavyo havikuwa na wagombea.Kuhusu hatima ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Vuai alisema itajulikana baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio.Alisema pamoja na CUF kujitoa, bado vyama vingine vina nafasi ya kushirikishwa katika serikali hiyo ikiwa vitapata nafasi ya kukidhi matakwa ya kikatiba na kisheria baada ya kuchaguliwa na wananchi na kupata uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.Hata hivyo, alisema kuwa CCM ipo tayari kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa na chama chochote ambacho kitatimiza mashariti ya Katiba ya kupata zaidi ya asilimia 10 ya matokeo ya uchaguzi.

Chama Cha Mapinduzi Zanzibar (CCM), kimeitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi mkuu wa marudio na vilivyojiondoa kabla ya kufanyika uchaguzi huo Machi 20, mwaka huu.Msimamo huo ulitolewa jana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, Ofisi Kuu za CCM Kisiwanduwi, baada ya vyama vinane kutangaza kuwa vimejiondoa.Vuai alisema ZEC inapaswa kutangaza vyama vilivyothibitisha kushiriki uchaguzi wa marudio pamoja na vile vilivyojiondoa baada ya muda wa kuthibitisha kushitiki kumalizika  Febuari 11, mwaka huu.Alisema kuna baadhi ya wanasiasa wameanza kufanya vitendo vya udanganyifu kuwa hawatashirikiuchaguzi wa marudio wakati uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana, hawakusimamisha wagombea.Vuai alisema viongozi wa vyama vya UPDP na UMD wamekuwa wakiwadaganya wananchi na dunia kuwa hawatoshiriki uchaguzi wa marudio wakati hawakuwa na wagombea katika uchaguzi wa Oktoba25.“Kuna utapeli wa kisiasa unafanyika, utasema vipi umejitoa katika uchaguzi wakati hukusimamisha wagombea katika uchaguzi uliyofutwa na Tume ya Uchaguzi mwaka jana,hii ni hadaa na hila .”alisema Vuai.Hata hivyo alisema kuwa kujiondoa kwa baadhi ya vyama hakuna madhara wala upungufu wowote katika uchaguzi huo kwa kuwa suala la kushiriki au kutoshiriki ni jambo la hiari.Taarifa ya CCM imekuja baada ya vyama vinane vya siasa kutangaza hawatoshiriki uchaguzi wa marudio vikitala taarifa zao kuondolewa katika karatasi za wapiga kura kwa madai uchaguzi wa Oktoba 25 ulikuwa huru na wa haki.Vyama hivyo ni Chauma, CUF, DP, Demokrasia Makini, SAU, Jahazi Asilia, NRA pamoja na UPDP naUMD ambavyo havikuwa na wagombea.Kuhusu hatima ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Vuai alisema itajulikana baada ya kufanyika uchaguzi wa marudio.Alisema pamoja na CUF kujitoa, bado vyama vingine vina nafasi ya kushirikishwa katika serikali hiyo ikiwa vitapata nafasi ya kukidhi matakwa ya kikatiba na kisheria baada ya kuchaguliwa na wananchi na kupata uwakilishi ndani ya Baraza la Wawakilishi.Hata hivyo, alisema kuwa CCM ipo tayari kuunda serikali ya Umoja wa Kitaifa na chama chochote ambacho kitatimiza mashariti ya Katiba ya kupata zaidi ya asilimia 10 ya matokeo ya uchaguzi.

Hakuna maoni:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Kurasa