BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Mbeya limeazimia kuondolewa kwa matumizi ya fedha yasiyokuwa ya lazima, imeelezwa.Hatua hiyo ni pamoja na kufuta baadhi ya posho za vikao na chakula kwa wajumbe.Baraza pia limeazimia kuanza kutumia vema fedha hizo ikiwamo kupunguza changamoto mbalimbali zamaendeleo zinazowakabili wananchi hususan katika elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara.Azimio hilo lilifikiwa jana katika kikao maalumu cha kujadili na kupitisha bajeti ya fedha ya mwaka 2016/2017 kilichafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya jiji hilo.Meya wa Jiji la Mbeya, David Mwashilindi, alisema ilihalmashauri iweze kutoa huduma bora kwa wananchi ni vema matumizi ya fedha yasiyokuwa na lazima yakapunguzwa kama posho za baadhi ya vikao na chakula kwa wajumbe.“Halmashauri yetu inakabiliwa na changamoto nyingi za elimu, afya, maji na miundombinu ya barabara.“Ukiangalia kuna baadhi ya matatizo kama vile uhaba wa matundu ya vyoo, ukarabati wa majengo ya shule yapo ndani ya uwezo wetu ni vema tukapunguza matumizi ya fedha yasiyokuwa na ulazima katika kuyatimiza haya,”alisema Meya.Alisema haiwezekani wajumbe wakaketi kwenye kikao kwa saa sita au tano na kulipana posho na kula chakula ambacho kinatumia fedha wakati watoto shuleni wanakaa chini na kutumia vyoo ambavyo miundombinu yake ni mibovu na ni hatari kwa maisha yao.Jukumu la madiwani na watendaji wa serikali ni kuhakikisha wanasimamia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya shule za msingi na sekondari, hususan kuongeza matundu ya vyoo, madawati,madarasa, uwekaji wa sakafu, milango na madirisha.Akizungumzia suala hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mbeya, Dk. Samweli Lazaro, aliwataka madiwani hao kuhakikisha wanaondoa tofauti za siasa katika kutekeleza majukumu ya maendeleo.Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha wanananchiwote wananufaika sambamba na kukuza Pato la Taifa.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni